Ni ukweli kuwa kwa sasa Darassa ameyasogelea mafanikio aliyokuwa akiyatamani kwa muda mrefu. Rapper mkongwe wa muziki wa Hip Hop nchini, Professor Jay amemuandikia ujumbe hitmaker huyo wa Muziki wa kumpongeza kwa kazi nzuri anayoifanya na kumtaka kuendelea kukaza buti.Kupitia mtandao wa Instagram, Jay ameandika:Mdogo wangu @darassacmg Imani yako, Kutokukata tamaa na Struggle yako ya Usiku na Mchana ndio imekufanya ufikie hapo ulipofikia, Nakumbuka wakati unashoot Wimbo wako wa USIKATE TAMAA uliniambia unatamani ufikie level za juu kama zetu, Nami nilikwambia hakuna kinachoshindikana chini ya JUA Ukiset GOALS, kufanya kazi kwa bidii na SALA yote Yanawezekana, Naamini kwa style hii ya JIWE juu Ya JIWE, NDOTO yako inakwenda kuwa kweli, Cha MSINGI usiridhike na mafanikio haya..HUU ni mwanzo tuu na mafanikio makubwa zaidi yako at your DOOR, Keep your eyes open and Keep ya HEAD UP,SKY IS THE LIMIT, GO GET DEM… BLESS#ACHA MANENO WEKA MUZIKI@darassacmg @darassacmg






Baraka Da Prince Atangaza Music Label Yake, Itamsimamia Pia Lord Eyez na Naj.

Kwenye muziki, mdogo wako wa leo, anaweza kuwa bosi wako wa kesho. Kuanzia sasa, rapper mkongwe wa Nako 2 Nako na aliyekuwa mmoja wa members wa kundi la Weusi, Lord Eyez atakuwa chini ya usimamizi wa label mpya mjini – BANA, inayomilikiwa na Barakah The Prince.Barakah ameitangaza label yake hiyo Jumanne hii wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa TV. Muimbaji huyo wa Nisamehe amedai kuwa Lord Eyez ataungana na mpenzi wake, Naj kama wasanii wa label hiyo na kwamba hivi karibuni nyimbo zao zitatoka.Amedai kuwa lengo la kumchukua Lord Eyez ni kutokana na kukubali uwezo wake na pia kutumbuiza naye kwenye show kadhaa, amegundua kuwa ana mashabiki kibao.





Post a Comment

 
Top