Pop staa Ariana Grande anarudi mjini Manchester Uingereza kwaajili ya tamasha kubwa la muziki la kuchangia pesa kwaajili ya familia za watu waliopoteza maisha kwenye mlipuko wa bomu katika show 22 May 2017, kwenye ukumbi wa Manchester Arena.
Ariana na meneja wake Scooter Braun, wameanza kuwasiliana na wasanii wakubwa Uingereza na Marekani kupata ushirikiano wao katika tamasha hili linalotegemea kufanyika kwenye kumbi nne kubwa Uingereza, moja wapo ni kumbi Manchester Arena, palipolipuka bomu lililouwa watu 22 na kujeruhi 59.
Kampuni ya burudani ya Live Nation itatayarisha show hii.

Post a Comment

 
Top