Mashuhuda
wa ajali iliyosababisha kifo cha Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake
Tanzania (UWT) Mkoa wa Dodoma, Salome Kiwaya wamesema alikufa kutokana
na kushindwa kupewa msaada kwa haraka.
Walisema
baada ya ajali walisikia sauti za watu wakilia kuomba msaada lakini
ilichukua muda wa sasa tatu ndipo walipopata msaada wa kuokolewa
kutokana na ukosefu wa vifaa vya uokoaji.
Juzi
katika eneo la Emmaus mkoani hapa ilitokea ajali ya gari la Toyota Noah
na lori ambayo ilichukua maisha ya Mwenyekiti huyo na watu wengine
watatu kujeruhiwa.
Mmoja wa mashuhuda hao Amri Juma alisema alisikia sauti za wanawake wakiomba msaada ili waweze kuokolewa.
“Ni
jambo la kusikitisha kuona zaidi ya saa tatu hakuna vifaa vya uokoaji
vilivyokuwa vimefika kwa ajili ya uokoaji, ajali ilitokea saa nane
mchana lakini mpaka saa 11 jioni ndio watu wanakuja kutolewa.
Post a Comment